Jamaa mmoja aliyemchinja mkewe na kumuua kabla ya jaribio lake la kujitoa uhai kutibuka ameachiliwa na mahakama moja nchini Uingereza, baada ya kutopatikana na hatia ya kuua kimaksudi.
Graham Mansfield, kutoka mji wa Manchester nchini Uingereza ameeleza mahakama jinsi alivyomchinja mkewe kwa jina Dyanne aliyekua na umri wa miaka 71 sababu ya mapenzi makubwa kwake, baada ya kumuona akiteseka akiugua ugonjwa wa saratani.
Mansfield amejitetea kuwa mkewe ndiye aliyemuomba amtoe uhai ili apumzike mateso na maumivu ya kuugua saratani isiyo na tiba na alimuahidi pia yeye atajiua ili waendeleze ndoa kuzimu; lakini jaribio lake la kujitoa uhai halikufanikiwa.
Mahakama imeamua kwamba Mansfield hakuua kimaksudi bali alilazimishwa kutekeleza mauaji na kumpatia “kifungo-hewa” cha miaka miwili, ambacho atakitumikia iwapo tu atafanya kosa lengine lakini kwa sasa yupo huru.