Afisaa mkuu mpya wa shirika la kusimamia haki miliki ya muziki humu nchini Ezekiel Mutua amewaahidi wasanii kwamba atapambana vilivyo kuwapigania haki zao.
Kupitia mitandao yake ya kijamii, Ezekiel amesema kwamba atashirikiana vilivyo na wasanii wa mziki kuhakikisha kwamba wanapata faida wanayostahili kutokana na kazi zao.
Kulingana na Ezekiel ni kwamba atawahusisha wasanii katika kila hatua ya majukumu yake ili kuhakikisha kwamba yote yanayowahusu wasanii moja kwa moja yanashughulikiwa.