Gumzo limezuka mitandaoni baada ya mpenzi mpya wa Rapper Kanye West muigizaji Julia Fox, kufuta picha zote ambazo yuko Pamoja na rapper huyo kwenye mtandao wa instagram.
Tukio hili limezua gumzo kubwa kwenye mitandao mbali mbali huku mashabiki wa wawili hao wakibaki na wasiwasi kwamba huenda mahusiano ya wawili hao yamegonga mwamba.
Hata hivyo Fox baada tu ya tukio hilo ameamua kuweka wazi kwamba tukio hilo halihusiani kamwe na mahusiano yake na Kanye West na ameamua kufuta picha hizo ili kurekebisha ukurasa wake wa Instagram.