Polisi wa eneo bunge la Kilifi Kaskazini kaunti ya Kilifi wanamenasa pombe haramu yenye thamani ya shilingi milioni 2.
Kulingana na kaimu kamishina kaunti ya Kilifi na Geofry Tanui pombe hiyo aina ya chan’gaa na kangara zaidi ya lita 10,000 inatengenezwa katika mazingira ambayo sio mazuri na ni hatari kwa afya ya binadamu.
Akizungumza eneo la Zowerani wadi ya Tezo ambako wameharibu pombe hiyo, Tanui amewataka wakazi kutoa ripoti kwa idara husika ili wakomeshe uuzaji wa pombe haramu.
Kwa upande wake kamanda wa polisi eneo la Kilifi Kaskazini Jonathan Koech amesema pombe hiyo ni hatari kwa binadamu na akisema uchunguzi umeanzishwa wa kuwatafuta washukiwa na kupelekwa mahakani kufunguliwa mashataka.