Msanii Burna Boy wa nchini Nigeria anaendelea kuandikisha rekodi mpya katika ulimwengu wa mziki barani Afrika na tour yake ya ‘Love, Damini’ ambayo inaendelea nchini Marekani kwa sasa.
Burna Boy amekua akiweka historia ya kujaza kumbi na sehemu anapokwenda kutumbuiza na hivi punde ameweka rekodi mpya baada kujaza mashabiki zaidi ya 20,000 katika ukumbi kwa jina Farm Arena jimbo la Atlanta nchini Marekani.