Tajiri mmoja ameshangaza wengi baada ya kufichua kuwa mali yake yote anayomiliki hatairithisha wanafamilia yake, bali ataachia “Mungu”.
David Green mwenye umri wa miaka 80, anamiliki kampuni moja kwa jina Hobby Lobby inayomiliki zaidi ya maduka 1000 katika majimbo 47 nchini Marekani na yenye thamani ya dola za kimarekani $6.4 billion.
Green anasema mungu ndiye mmiliki halisi wa mali na utajiri wote duniani na hataki familia yake kurithi utajiri wake wowote bali mungu pekee.